Head image
Govt. Logo

Hits 110663 |  3 online

           


Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais amesema kuwa mashirikiano ya pamoja yanaleta maelewano katika sehemu ya kazi
news phpto

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Mhe Harusi Said Suleiman amesema kuwa mashirikiano ya pamoja yanaleta maelewano katika sehemu ya kazi na kukuza uhusiano mwema unaojenga imani na mapenzi baina yao

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Mhe Harusi Said Suleiman amesema kuwa mashirikiano ya pamoja yanaleta maelewano katika sehemu ya kazi na kukuza uhusiano mwema unaojenga imani na mapenzi baina yao

Mhe Harusi ameyasema hayo wakati alipofanya mazungumzo na wafanyakazi wa ofisi hio kwenye ukumbi wa mkutano uliopo Migombani na kuwasisitiza kuwa suala la nidhamu na heshima katika kazi ni jambo la msingi huku wakijua kuwa taifa linawategemea

Bi Harusi amesisitiza kuwa mashirikiano ya wenyewe kwa wenyewe yanawaleta karibu wafanyakazi na watendaji jambo ambalo linaleta ufanisi katika sehemu za kazi ndipo mipango ya utekelezaji na ujenzi wa taifa inapoendana na kasi ya utendaji

“hakikisheni mnajikita katika majukumu ya kazi na mmoja wenu anapoondoka majukumu hayalali bali kazi iendelee ndio maana nawasisitiza kupendana pia msifanye kazi kwa mazowea badala yake jitahidini kuleta ufanisi ili maendeleo yaweze kupatikana” alisisitiza Mhe Harusi

Aidha Bi Harusi amewakumbusha wafanyakazi kuzingatia muda wa kuingia na kutoka kazini na inapotokea hali ya dharura kutoa taarifa kwani si vyema kunyamza unaweza kupoteza haki zako za msingi mambo ambayo hayana tija kiutendaji

Kuhusu suala la uwajibikaji amewataka wafanyakazi kuhakikisha wanatoa huduma stahiki kwa jamii hivyo kila mfanyakazi afahamu majukumu yake pamoja na kuzingatia suala la utowaji wa huduma kwa walioko nje ya ofisi kuhakikisha wanafikiwa

Nae Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Kwanza wa Rais Dkt Omar D. Shajak amemuhakikishia Mhe Waziri kuwa nidhamu na mashirikiano ndio yenye kuleta uhai wa taasisi jambo viongozi wa Ofisi hio wanalisisitiza kwa watendaji na wafanyakazi wote

Huduma za Tehama

Barua Pepe

Sisi

Mwanzo Kuhusu Sisi Idara Zetu

Viunga Muhimu

ZEMA ZAC DDA IKULU

Mawasiliano

Ofisi Kuu
S.L.P 2808, Migombani, Zanzibar
Tel.: +255(24)2232474 Mhe Waziri



Tel.: +255 (24)2232475 Katibu Mkuu,
Fax: +255 (24)2232476
Email: info@omkr.go.tz